Posts

MAWAKILI WA SERIKALI, MAAFISA SHERIA KUTOA HUDUMA ZA MSAADA WA KISHERIA ILI KUONGEZA WIGO WA UPATIKANAJI HUDUMA

Wizara ya Katiba na Sheria imeandaa Mpango utakaowawezesha Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria ambao ni Mawakili wa Kujitegemea au wana sifa za kuwa Mawakili wa Kujitegemea kuruhusiwa kutoa huduma za msaada wa kisheria hususani uwakilishi kwa mashauri ambayo hayana mgongano wa kimaslahi na mwajiri. Akifungua rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria leo 28 Januari, 2026 jijini Arusha, Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA. Amos Makalla akimuwakilisha Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera amesema kuwa Mpango huu utawawezesha Mawakili na Maafisa Sheria kutoa huduma za msaada wa kisheria kwa jamii ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma, kuweka uendelevu wa huduma na kuimarisha ufanisi na utendaji katika kazi za sheria. Mh. Makalla amesema kuwa ni wajibu wa Mawakili wa Serikali kuhakikisha wanaongeza uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya haki na wajibu wao kwa lengo la kuendelea kujenga Taifa lenye amani na maendeleo. “Uhitaji wa huduma za msaada wa kisheria kwa...

DKT. MWIGULU AONGOZA MKUTANO WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA BUNGE

Image
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo January 28,2026 ameongoza Mkutano wa Kamati ya Katiba, Sheria na Bunge ya Baraza la Mawaziri kwenye ukumbi wa Spika, bungeni jijini Dodoma, Januari 28, 2026.

Benki ya NMB yashiriki kwenye ufunguzi wa Wiki ya Vijana inayofanyika Kitaifa Mbeya

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa na baadhi ya Wadhamini wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yaliyozinduliwa Oktoba 10,2025 akiwemo Meneja Mahusiano Mwandamizi wa NMB Josephine Kulwa wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Vijana katika Soko la Uhindini jijini Mbeya. Baadhi ya wanafunzi na wananchi waliohudhuria ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana Oktoba 10,2025 katika Viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya wakifuatilia kwa karibu hotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa aliyekuwa mgeni rasmi. Wanafunzi wa shule ya Sekondari wasichana Loleza waliotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya Vijana viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya. Matukio mbalimbali katika picha kwenye Banda la NMB Oktoba 10,2025 wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya.

WAHIFADHI MNA DHAMANA YA KULINDA RASILIMALI ZA TAIFA- RC MAKALLA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amewataka Watumishi na Viongozi wa Mamlaka za hifadhi za Taifa zilizopo Mkoani Arusha kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kwa uzalendo, wakitambua kuwa wanayo dhamana kubwa ya kulinda rasilimali za nchi na uendelevu wa Vivutio vya Utalii vilivyopo Arusha. CPA Makalla ameyasema hayo leo Jumamosi Septemba 20, 2025 Mto wa Mbu Karatu kwenye Makao Makuu ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, alipokutana na kuzungumza na Menejimenti ya Shirika la hifadhi ya Taifa TANAPA, akiwataka pia kuwa Mabalozi wazuri wa kusukuma mbele jitihada za Rais wa Awamu ya Sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kukuza utalii wa Mkoa wa Arusha na Tanzania. "Nyie ni mabalozi wetu wazuri na tunawaamini, hakikisheni mnalinda hifadhi tulizonazo, mkitimiza majukumu yenu kwa uadilifu na uzalendo kwa nchi yenu. Utalii ni matokeo ya uhifadhi, tuunge Mkono jitihada za Mhe. Rais ambazo zimetusaidia kuwa na Ongezeko kubwa la Idadi ya watalii kwenye Hifadhi tulizonazo....

MWALUNENGE ATETA NA SHIRIKISHO LA WALIMU MAKADA WA CCM MKOA WA MBEYA

Image
Mgombea Ubunge kupitia Jimbo la Mbeya Mjini na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya Patrick Mwalunenge  tarehe 20 Septemba 2025 amekutana na Shirikisho la Walimu Makada wa CCM mkoa huo na kuwaomba kutafuta kura za heshima za Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt.Samia Suluhu Hassan  Wabunge pamoja na Madiwani wote wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Mbeya

RC CHALAMILA AZINDUA KLINIKI MAALUM HOSPITALI YA MLOGANZILA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila Septemba 18, 2025 amezindua "Premier Clinic " katika Hospitali ya Mloganzila Wilaya ya Ubungo Jijini Dar es Salaam. Akiongea wakati wa uzinduzi huo mapema leo RC Chalamila amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya Afya, kwa kuwa sasa Hospitali nyingi zina miundombinu mizuri, wataalamu wazuri, pamoja na vifaa tiba. " Hakika huo ni uwekezaji mkubwa" Aidha RC Chalamila ameipongeza Hospitali ya Mloganzila kwa kuwa wabunifu kuanzisha kliniki maalum (Premier Clinic) ambayo inakwenda kutoa huduma za kibingwa na ubingwa bobevu katika upandikishaji wa Figo, Uloto, nyonga, uchunguzi na matibabu ya ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu. Vilevile upasuaji wa uti wa mgongo kwa watoto, matibabu ya saratani, huduma za upasuaji rekebishi, huduma za dharura na ajali, uchunguzi na matibabu ya mafuta kwenye mishipa ya damu pamoja na matibabu ya kis...

MWALUNENGE AMNADI DIWANI DORMOHAMED

Image
Mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Patrick Mwalunenge 18 Septemba 2025 amemnadi Mgombea Udiwani Kata ya Isanga jijini Mbeya DorMohamed Issah na kuwaomba wakazi wa kata hiyo kutofanya makosa ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025 kumpa  kura za heshima Rais Samia yeye mwenyewe Mgombea Ubunge  na Madiwani wote wa Chama Cha Mapinduzi akiwemo Dormohamed kupiga  kura za heshima ili Chama Cha Mapinduzi kiweze shika dola na baadae kiweze kuwaletea maendeleo wanaisanga pamoja na wakazi wa Mbeya Mjini kwa ujumla. Mwalunenge pia amewahidi wakazi wa kata ya Isanga endapo watampa kura za heshima na kuwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini atahakikisha soko la kata hiyo linakwenda kuboreshwa ikiwemo kuwafungia wakinamama wenye watoto wachanga  vitanda vya kupumzikia (DayCare) na kutowabuguzi wazazi pindi wafanyapo biashara zao