Posts

MAKALLA AMKARIBISHA CCM MCHUNGAJI MSIGWA

Image
 

DIWANI ADAM SIMBAYA AGAWA UPENDO KWA WAJUMBE WDC MBALIZI ROAD

Image
Diwani Kata ya Mbalizi Road Jijini Mbeya Mhe Adam Simbaya awashukuru  Wajumbe wa WDC Kata ya Mbalizi Road kwa ushirikiano mkubwa wanaotoa  katika Kata hiyo. Hayo ameyaongea  katika Kikao cha WDC kilichofanyika  Matema Beach Wilayani Kyela na  kuwashukuru Wajumbe hao kwa  ushirikiano walioutoa kwa kipindi chote. Pamoja na Kuwaaga Wenyeviti ambao  wanamaliza   muda wao,  Mhe Diwani alitoa zawadi  kwa wenyeviti wake wote wa Mitaa Minne kwa niaba ya WDC ikiwa ni  kumbukumbu yao kwa kipindi ambacho kimebakia kumalizia nafasi ya wenyeviti wa mitaa

MABADILIKO YA KWELI YATALETWA NA MATUMIZI SALAMA YA MIFUMO YA KAZI KWA WATUMISHI

Image
Maneno hayo pamoja na ushauri juu ya mienendo ya kiutendaji miongoni mwa Maafisa RasilimaliWatu yamesemwa na Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora Ndg. Ridhiwani Kikwete J. alipokuwa anafunga Mkutano wa 11 wa wanachama wa Chama Cha Maafisa Tawala na Rasilimali Watu (AAPAM) uliofanyika katika Ukumbi wa AICC , jijini Arusha. Naibu Waziri Kikwete, ameelekeza Maafisa hao kuendelea kutumia mifumo ya utendaji kazi ili kuwezesha  haki na wajibu  kutolewa kwa watumishi wa umma. Akizungumza na watumishi hao katika siku ya mwisho ya Mkutano huo wa siku tatu, Ndugu Kikwete aliwakumbusha watumishi hao mifumo mbalimbali iliyokwisha tengenezwa kuwezesha watumishi kukopa, kuhama na kupima utendaji kazi. Katika hali nyengine , Naibu Waziri Kikwete amewaonya Maafisa hao juu ya tabia inayoendelea ya kutowatendea vyema watumishi wenzao wanaowaongoza.  Naibu Waziri ameonya juu ya roho mbaya walizonazo baadhi ya Watendaji hao akitoa mfano wa Rorya na taratibu za upandishaji madaraja.

MAHUNDI AKABIDHI NONDO 50 ZA UJENZI WA OFISI YA CCM KATA YA MBALIZI ROAD JIJINI MBEYA

Image
Naibu Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mhandisi Maryprisca Mahundi amekabidhi msaada wa nondo zaidi ya hamsini kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)Mbalizi Road Jijini Mbeya. Nondo hizo zimekabidhiwa na Lucia Mwanasinjale Katibu wa Mbunge ambaye pia ni Diwani wa Viti Maalumu Jiji la Mbeya kwa niaba ya Mbunge. Naye Mratibu wa ofisi ya Mbunge Fatuma Bora amesema huu ni utekelezaji wa ombi la Kata ya Mbalizi Road lililoombwa kwa Mbunge na Viongozi wa Kata. Sophia Malingumu Mjumbe kamati ya siasa Kata ya Mbalizi Road amemshukuru Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mhandisi Maryprisca Mahundi kwa mchango mkubwa kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa ofisi ya Chama. Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mbalizi Road Mheshimiwa Adam Simbaya amesema Mheshimiwa Mahundi aliombwa kuchangia nondo thelathini lakini yeye ametoa nondo hamsini ikiwa ni zaidi ya kiwango kilichoombwa. "Hii itakuwa ofisi ya mfano nch...

HOSPITALI YA RUFAA KANDA MBEYA YANG'ARA MEI MOSI KITAIFA

Image
Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imeendelea kung'ara na kuvunja rekodi kwa kutoa wafanyakazi hodari kwa vipindi viwili (mwaka 2022 na 2024). Hatua hii imefikiwa baada ya mfanyakazi hodari Joshua J. Kusaga, Fundi Sanifu vifaa tiba, kuchaguliwa kuwa mfanyakazi hodari Mei Mosi kitaifa. Katika hafla iliyofanyika jijini Arusha, Joshua alikabidhiwa zawadi na Makamu wa Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika sherehe hizo. Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya inajivunia kuwa na wafanyakazi wenye uwezo mkubwa na inaendelea kuweka msisitizo katika kutoa huduma bora za afya kwa wananchi. Mfanyakazi huyu ameonyesha uwezo, bidii na utaalamu wa hali ya juu katika kutekeleza majukumu yake. Tunampongeza Joshua J. Kusaga kwa mafanikio haya makubwa na tunamtia moyo kuendelea kufanya kazi kwa bidii na uaminifu ili kuendelea kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya afya nchini.

Dkt.Tulia azindua kituo cha Afya cha Chaani

Image
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mikoa ya Kaskazini na Kusini Unguja,  Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 27 Aprili, 2024 amezindua na kufungua Kituo cha Afya cha Chaani katika Jimbo la Chaani, Wilaya ya Kaskazini A kilichojengwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Nadir Alwardy. Wakati wa uzinduzi huo, Dkt. Tulia pia ametoa msaada wa Shilingi Milion 10 kwa waathirika wa mafuriko yaliyosababishwa na mvua hivi karibuni katika Mkoa wa Kaskazini, Zanzibar.